Posts

Showing posts from February, 2024

KUNDI LINGINE LA WANANCHI 541 LAHAMA NGORONGORO

Image
KUNDI LINGINE LA WANANCHI 541 LAHAMA NGORONGORO Na Mwandishi wetu, NCAA. Hamasa ya  wananchi wanaojiandikisha kuhama kwa hiyari kutoka eneo la hifadhi ya Ngorongoro  imeongezeka ambapo leo tarehe 19 February , 2024 jumla ya kaya 82 zenye wananchi 541 na mifugo 3,379 zimehama kutoka Ngorongoro kweda Kijiji cha Msomera Handeni Tanga. Akizungumza wakati wa kuaga kundi hilo Kamishna wa Uhifadhi wa NCAA Richard Kiiza amesema kuwa baada ya kuhama kwa kundi hilo leo inafanya idadi ya wananchi waliokwishahama ndani ya hifadhi tangu zoezi lilipoanza hadi leo kufikia kaya 1,032 zenye watu 6,395 na mifugo 28,982. Kamishna Kiiza amebainisha kuwa kadri siku zinavyoenda wananchi wengi wanahamasika na kujiandikisha kuhama kwa hiari yao wenyewe hasa baada ya ushuhuda wa maisha mazuri kwa wananchi wenzao waliokwishatangulia ambao Maisha yao yamebadilika kwa kiasi kikubwa. “Wananchi waliotangulia mwaka jana wengi wao wamejenga nyumba za kisasa, wamelima mazao ya kutosha kwa ajili ya chakula na ...

UTALII WA MALIKALE WASHIKA KASI NCHINI, WAFARANSA WAFURIKA KILWA KISIWANI

Image
UTALII WA MALIKALE WASHIKA KASI NCHINI,  WAFARANSA WAFURIKA KILWA KISIWANI   Na Beatus Maganja Kwa miongo kadhaa kumekuwa na dhana ya kwamba wageni wengi wa nje hupendelea zaidi utalii wa kuona wanyamapori, lakini hivi karibuni dhana hiyo imeanza kubadilika kwa kasi ambapo Tanzania imeanza kupokea wageni makundi kwa makundi wakitembelea katika maeneo yetu ya Malikale hususan Hifadhi ya Urithi wa Dunia ya Magofu ya Kilwa kisiwani na Songo Mnara. Ni takrikani siku 9 sasa katika kipindi cha Mwezi Februari kuanzia tarehe 03 - 11, 2024, Tanzania kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA imeweza kushuhudia   Meli zilizosheheni makundi ya Watalii kutoka Mataifa mbalimbali zikipishana kutia nanga katika Hifadhi ya Urithi wa Dunia ya Magofu ya Kilwa kisiwani na Songo Mnara na kufikisha idadi ya watalii wapatao 445 kwa safari nne (4) za kitalii zilizofanyika. Kwa mara nyingine Februari 11, 2024 TAWA ilipokea kundi la nne (4) la watalii wapatao 114  kutoka Ufa...

RAIS SAMIA ARIDHIA KUANZISHWA KWA MTAALA WA MASOMO YA UTALII

Image
RAIS SAMIA ARIDHIA KUANZISHWA KWA MTAALA WA MASOMO YA UTALII Na Happiness Shayo-Dodoma Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia kuanzishwa kwa masomo ya Utalii kwa kidato cha tano na sita nchini lengo ikiwa ni kuendelea kuikuza Sekta ya Utalii. Hayo yamesemwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) katika kikao kati yake na Wabunge wa Mikoa ya Kilimanjaro na Tanga kilichofanyika ukumbi wa Utawala Bungeni jijini Dodoma leo. “Tunashukuru Mheshimiwa Rais aliona umuhimu wa kuanzishwa kwa mchepuo wa masomo ya utalii na hakuchukua muda mrefu kulikubali suala hilo” Mhe. Kairuki amesisitiza. Amesema lengo la kuanzishwa kwa mchepuo wa masomo ya utalii ni kuendelea kuiboresha sekta hiyo akitolea mfano kutoa mafunzo ya utoaji wa huduma kwa wateja, lugha na kadhalika. Amesema ameshawasilisha toolkit ya mchepuo huo  ambayo inaendana na matakwa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani ( World Tourism Organization-UNWTO)pamoja n...

MELI YENYE WATALII ZAIDI YA 100 YATIA NANGA HIFADHI YA MAGOFU YA KALE KILWA KISIWANI

Image
  MELI YENYE WATALII ZAIDI YA 100 YATIA NANGA HIFADHI YA MAGOFU YA KALE  KILWA KISIWANI Na mwandishi wetu/Kilwa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA leo Februari 03, 2024 imepokea meli kubwa ya watalii wapatao 102 kutoka uingereza waliofika katika Hifadhi ya Urithi wa Dunia ya Magofu ya Kilwa kisiwani na Songo Mnara kwa ajili ya shughuli za utalii kisiwani humo. Watalii hao wakiongozwa na Kampuni ya Utalii ya Takim Holidays walipokelewa na kukaribishwa kwa ngoma za asili ya watu wa Kilwa Kisiwani iitwayo kitupolo ambayo iliwafanya waonekane wakifurahi muda wote. Ngome ya Mreno, Msikiti mkubwa na mkongwe, Makaburi ya Malindi na Makutani Palace ni miongoni mwa maeneo yaliyotembelewa na watalii hao ikiwa ni pamoja na kupata fursa ya kujifunza tamaduni za watu wa Kilwa kisiwani. Historia na upekee wa Hifadhi hii ya Magofu ya Kilwa kisiwani na Songo Mnara imekuwa kivutio kikubwa cha watalii kutoka Kona mbalimbali za Dunia ambao hutembelea Hifadhi hiyo Karibu Kila Mwa...

SHIRIKA LA CTG - CHINA KUSHIRIKIANA NA TANZANIA KUTANGAZA UTALII

Image
SHIRIKA LA CTG - CHINA  KUSHIRIKIANA NA TANZANIA KUTANGAZA UTALII  Na Happiness Shayo Shirika la Kiserikali la China linalosimamia utangazaji wautalii  na uwekezaji  (China Tourism Group - CTG) limeonesha nia ya kutaka kutangaza vivutio vya utalii vilivyoko nchini Tanzania pamoja na kuwekeza katika maeneo mbalimbali ya Sekta ya Utalii nchini kwa  lengo la  kukuza utalii wa Tanzania na kuongeza mapato yatokanayo na Sekta hiyo. Hayo yamesemwa leo Februari 1,2024 na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) katika kikao kati ya shirika hilo pamoja na Watendaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii kilichofanyika Jijini Dodoma. Akizungumza katika kikao hicho, Waziri Kairuki amesema  Tanzania itanufaika na ushirikiano huo ambapo moja ya kipaumbele cha Serikali kwa sasa ni kuvutia watalii wengi kutoka nchi za nje hivyo, Serikali itatumia fursa hiyo kuvutia watalii kutoka soko la China. Aidha, Mhe. Kairuki ameliomba  Shirika hilo kuwekeza kati...