Posts

Showing posts from January, 2024

MWAROBAINI WA MIUNDOMBINU KOROFI SERENGETI WAPATIKANA

Image
  MWAROBAINI WA MIUNDOMBINU KOROFI SERENGETI WAPATIKANA      Na. Edmund Salaho/Serengeti. Kamishna wa Uhifadhi - TANAPA Juma Kuji leo amefanya ziara ya kukagua miundombinu katika Hifadhi ya Taifa Serengeti na kuiagiza Menejimenti ya Hifadhi ya Taifa Serengeti kushughulikia mara moja maeneo korofi ya barabara ndani ya hifadhi hiyo, ili watalii wafikie adhma yao ya kutembelea Hifadhi ya Taifa Serengeti. Akizungumza baada ya kukagua maeneo hayo Kamishna Kuji, ameielekeza Menejimenti ya Hifadhi ya Taifa Serengeti kurekebisha maeneo yote korofi na kuhakikisha kuwa hakuna maeneo ambayo hayatapitika licha ya uwepo wa mvua kubwa zinazoendelea kunyesha ili kupunguza adha kwa wageni. “Licha ya changamoto ya mvua kubwa zinazoendelea hatuwezi kusubiri ziishe tumeazimia kushughulikia kwa haraka maeneo yote korofi ikiwa ni hatua za haraka, lakini lengo kuu ni kuhakikisha  barabara hizi zinakuwa na tabaka gumu, haya ni maagizo yangu kwa menejimenti kuhakikisha barabara zote zi...

TTB NA TANAPA WATANGAZA UTALII WA TANZANIA KATIKA MAONESHO YA FITUR - MADRID

Image
TTB NA TANAPA WATANGAZA UTALII WA TANZANIA KATIKA MAONESHO YA FITUR - MADRID   Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia taasisi zake za TANAPA  na TTB wanashiriki Onesho la Fitur - Madrid Hispania kwa lengo la kunadi na kuhamasisha watalii wengi zaidi kutembelea vivutio vya utalii vinavyopatikana Tanzania. Onesho hilo linatarajiwa kuwa na washiriki zaidi ya 220,000 kutoka mataifa mbalimbali duniani. Katika Onesho hilo pia TANAPA inaendelea kunadi fursa za uwekezaji zinazopatikana  ndani ya hifadhi hizo. Aidha, onesho hilo mbali na kuwashirikisha TTB na TANAPA pia limewajumuisha wadau wa utalii na limeanza tarehe 24.01.2024 na linatarajiwa kuhitimishwa tarehe 28.01.2024 .

HAKUNA MWANANCHI WA NGORONGORO ATAKAYEKOSA HAKI YAKE-RC MONGELLA

Image
 HAKUNA MWANANCHI WA NGORONGORO ATAKAYEKOSA HAKI YAKE-RC MONGELLA  Na mwandishi Wetu, NCAA Mkuu wa Mkoa wa Arusha mheshimiwa John Mongella amewahakikishia wananchi wanaohama kwa hiari kutoka ndani ya hifadhi ya Ngorongoro kwenda maeneo mengine nje ya hifadhi  kuwa serikali imejipanga na hakuna mwananchi yoyote atakayekosa haki zake iwapo ataamua kuhama kwa hiyari. Mheshimiwa Mongella ametoa kauli hiyo wilayani Ngorongoro Mkoani Arusha leo tarehe 25 Januari, 2024 wakati akiwaaga wananchi 818 walioamua kuhama kwa hiyari kutoka ndani ya hifadhi hiyo na kwenda kuishi katika Kijiji cha Msomera wilayani Handeni Mkoani Tanga. Ameeleza kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt .Samia Suluhu Hassan ametoa fedha za kutosha ili kuhakikisha kuwa zoezi hilo linafanikiwa na  hakuna mwananchi yoyote atakayekosa kulipwa haki zake zote zilizoanishiwa katika utekelezaji wa zoezi hilo. Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa ameongeza kuwa zoezi hilo linatekelezwa kwa kuzingatia misingi yote...
Image
  TAWIRI  NA MUENDELEZO WA TAFITI UGONJWA WA TWIGA ULIOATHIRI ASILIMIA 62 YA TWIGA KATIKA HIFADHI YA TAIFA RUAHA Na Mwandishi wetu, Arusha Taasisi ya Utafiti wa  Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) inaendelea kufanya  tafiti zaidi juu ya madhara na matibabu ya ugonjwa wa ngozi wa Twiga ambao  matokeo ya awali yameonyesha maeneo yanayoathirika ya viungio kwenye miguu (magoti) hususan miguu ya mbele, kuna vimelea vya bakteria, virusi na fangasi. Akizungumza wakati wa ufuatiliaji wa matibabu ya ugonjwa huo katika hifadhi ya Taifa Ruaha, Dkt. Julius Keyyu ambaye ni  Mkurugenzi wa Utafiti  TAWIRI,  amesema ugonjwa wa ngozi wa Twiga uliogundulika katika hifadhi  ya Taifa  Ruaha mwaka 2000 ni tofauti na ugonjwa wa ngozi wa Twiga katika nchi nyingine duniani  " tumefuatilia ugonjwa huu kwa nchi nyingine duniani na kubaini upo tofauti na hapa nchini" amebainisha  Dkt. Keyyu Dkt.Keyyu amesema asilimia  62% ya Twiga waliopo hifadhi ya ...
Image
MAKAMU WA RAIS WA CUBA AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba, Mhe. Salvador Valdés Mesa amewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 23 - 25 Januari, 2024.  Mara baada ya kuwasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Mhe. Mesa alipokelewa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb.) Akiwa nchini, Mhe. Mesa atakutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete na pia atatembelea taasisi ya Mwalimu Nyerere. Mhe. Mesa pia atamtembelea Mjane wa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Mama Maria Nyerere pamoja na kutembelea kiwanda kinachozalisha dawa za viuadudu ya Biolarvicide cha Kibaha, Pwani.
Image
 TANAPA YANUFAIKA NA SOKO LA KIMKAKATI LA UTALII ZANZIBAR Na. Jacob Kasiri, Zanzibar. Kamanda wa Uhifadhi Kanda ya Kusini - TANAPA, Steria Ndaga amesema uwepo wa Soko la Kimkakati la Utalii Zanzibar limechangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la watalii katika Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) hususan, Hifadhi za Taifa Kanda ya Kusini na Mashariki ukilinganisha na miaka ya nyuma ambapo wageni wengi walikuwa wakitoka ukanda wa Kaskazini. Kamanda huyo ameyasema hayo leo tarehe 19.01.2024 kisiwani Zanzibar. Akiwa katika Viwanja vya Maonesho ya 10 ya Biashara ya Kimataifa Fumba - Zanzibar, Kamanda Ndaga alisema,  "Maonesho haya ni sehemu ya mkakati wetu na wadau wa utalii kuhakikisha vifurushi vinavyouzwa katika Hifadhi za Taifa vinakuwa na idadi kubwa ya watalii wanaotumia muda mwingi hifadhini ili kuliongezea taifa mapato." Itakumbukwa mwishoni  mwa mwezi Agosti, 2023 Kamisheni ya Utalii Zanzibar (ZCT) na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) walisaini mkataba wa ushirikiano wa kutanga...