Posts

RAIS DKT. SAMIA: BARABARA MPYA YA TANGA, PANGANI, SAADANI NA BAGAMOYO KUIFUNGUA TANGA KIUTALII

Image
Na Philipo Hassan - Tanga Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, alisema kuwa kukamilika kwa barabara ya lami inayounganisha Tanga, Pangani, Saadani na Bagamoyo pamoja na Daraja la Mto Pangani lenye urefu wa mita 525 zitasaidia kuifungua Tanga Kiutalii na kiuchumi. Rais Samia ameyasema hayo leo, Februari 26, 2025 wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi katika ujenzi wa  barabara na Daraja la Mto Pangani ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa ziara yake mkoani Tanga. Vilevile, alisisitiza kuwa miundombinu hiyo mipya itarahisisha maeneo mengi ya utalii kufikika kiurahisi. Rais Samia alieleza โ€œBarabara hii tunayoiunganisha inaenda kuifungua Tanga kiutalii na kibiashara. Maeneo mbalimbali ya kiutalii ambayo hayafikiki, itakuwa ni rahisi kumtoa mtalii Hifadhi ya Taifa Saadani na kwenda kutalii maeneo mengine ndani ya Mkoa wa Tangaโ€  Naye, Mbunge wa jimbo la Pangani Mhe. Jumaa Aweso alimshukuru Rais Samia kwa kutekeleza mradi mkubwa wa barabara na Daraja ambayo yat...

SIX RIVER AFRICA NA ECO WASHIRIKIANA NA TANAPA KUBORESHA HUDUMA ZA MATIBABU YA WANYAMAPORI

Image
Na. Happiness Sam- Same Shirika la Six Rivers Africa pamoja na Elephant Conservation Organisation (ECO) yameungana na TANAPA ili kuimarisha huduma za matibabu ya wanyamapori katika hifadhi za kanda ya kaskazini kwa kuongeza vitendea kazi ikiwemo gari, vifaa tiba pamoja na dawa za kutibu wanyamapori ili kuhakikisha ustawi wa wanyamapori unaimarika katika maeneo hayo. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Mradi wa Tiba ya Wanyamapori, jana Februari 18, 2025 katika Hifadhi ya Taifa Mkomazi iliyopo Wilaya ya Same, Mkoani Kilimanjaro, Mkuu wa wilaya ya Same Kasilda Mgeni alieleza umuhimu wa uhifadhi kwa maendeleo ya taifa kwani unasaidia katika kutunza urithi wetu wa asili ikiwemo wanyamapori kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vizazi vijavyo. DC Mgeni alisema  โ€œMradi wa Tiba ya Wanyamapori (Veterinary Support Project) ulianzishwa mwaka 2013 katika Hifadhi yetu ya Taifa ya Mkomazi kwa lengo la kuchukua hatua muhimu katika kuhakikisha mafanikio endelevu ya juhudi zetu za uhifadhi, mradi ...

WAZIRI CHANA AFUNGUA RAS ONESHO LA WIKI YA UBUNIFU LA ITALIA JIJINI DAR ES SALAAM

Image
โ€ข Aipongeza Italia kwa mashirikiano katika sekta ya utalii Na Happiness Shayo- Dar es Salaam Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) amefungua rasmi Onesho la Wiki ya Wabunifu wa Italia linaloonesha picha za wabunifu mbalimbali wakubwa wa zamani kutoka nchini Italia na  kuipongeza nchi hiyo kwa ushirikiano kati yake na Tanzania kwenye sekta ya utalii. Ufunguzi huo umefanyika  leo Februari 10,2025 katika Kituo cha Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Jijini Dar es Salaam ambapo onesho hilo linatarajiwa  kumalizika Februari 20,2025 likiwa na lengo la kukuza ushirikiano katika masuala ya utalii, historia na uchumi.  โ€œ Italia imejitolea katika juhudi zetu za kukuza utalii endelevu na kuhifadhi urithi wetu wa asili na kiutamaduni .Mfano mmoja mzuri wa ushirikiano huu ni mradi wa Kisiwa cha Bawe, ambao ni mwanzo mzuri unaoonyesha utalii endelevu. Mradi huu hauangazii tu uzuri wa visiwa vya Tanzania bali pia unaonesha matokeo chanya ya uwekezaji wa ki...

๐“๐€๐๐€๐๐€ ๐‚๐ž๐ฅ๐ž๐›๐ซ๐š๐ญ๐ž๐ฌ ๐…๐ข๐ฏ๐ž ๐‚๐จ๐ง๐ฌ๐ž๐œ๐ฎ๐ญ๐ข๐ฏ๐ž ๐–๐ข๐ง๐ฌ ๐จ๐Ÿ ๐๐ฎ๐š๐ฅ๐ข๐ญ๐ฒ ๐‚๐ก๐จ๐ข๐œ๐ž ๐๐ซ๐ข๐ณ๐ž ๐Ÿ๐จ๐ซ ๐„๐ฑ๐œ๐ž๐ฅ๐ฅ๐ž๐ง๐œ๐ž ๐ข๐ง ๐’๐ž๐ซ๐ฏ๐ข๐œ๐ž ๐ƒ๐ž๐ฅ๐ข๐ฏ๐ž๐ซ๐ฒ

Image
Tanzania National Parks (TANAPA) has been honored with the prestigious Quality Choice Prize 2024 in recognition of its exceptional commitment to delivering world-class services within and beyond the organization. The award ceremony, organized by the European Society for Quality Research (ESQR), took place on December 9, 2024, at Parkhotel Schรถnbrunn in Vienna, Austria. The award was received by the Deputy Minister of Natural Resources and Tourism for Tanzania, Hon. Dustan Kitandula, who was accompanied by Ambassador of United Repblic of Tanzania in Vienna Austria, Hon. Naimi Aziz, TANAPAโ€™s Conservation Commissioner Musa Juma, Western Zonal Senior Conservation Commissioner Izumbe Msindai, Conservation Commissionerโ€™s Personal Assistant Andrew Mbai, and Conservation Officer from the Business Development Section, Daniel Mweta. This remarkable achievement marks TANAPAโ€™s fifth consecutive win of the Quality Choice Prize from 2020 to 2024, underscoring its continued excellence in quality mana...

TANZANIA SIGNS โ‚ฌ39.9M DEAL TO BOOST FOREST PLANTATION AND MANGROVE CONSERVATION

Image
Dar es Salaam; December 6, 2024: Tanzania has signed a โ‚ฌ39.9 million agreement with the French Development Agency (AFD) to strengthen the management of government forest plantations and conserve mangrove forests. The project aims to enhance the economic and ecological value of the forestry sector while addressing critical challenges. Speaking during the signing ceremony at the Treasury Building in Dar es Salaam, Hon. Dunstan Kitandula, the Deputy Minister for Natural Resources and Tourism, hailed the project as a testament to the government's commitment under President Samia Suluhu Hassan to conserve and develop Tanzania's forestry sector. Tanzania's Mainland boasts 48.1 million hectares of forest, covering 55% of its land area, yet only 120,000 hectares of plantation forests have been developed out of a potential 583,691 hectares. The project aims to address this gap by planting 22,500 hectares of trees over five years in Silayo, Mtibwa, and Wino farms. Additionally, it wi...

๐”๐‰๐„๐๐™๐ˆ ๐–๐€ โ€œ๐’๐„๐‘๐„๐๐†๐„๐“๐ˆ ๐๐€๐“๐ˆ๐Ž๐๐€๐‹ ๐๐€๐‘๐Š ๐†๐Ž๐‹๐… ๐‚๐Ž๐”๐‘๐’๐„โ€ ๐–๐€๐…๐ˆ๐Š๐ˆ๐€ ๐€๐’๐ˆ๐‹๐ˆ๐Œ๐ˆ๐€ ๐Ÿ’๐Ÿ

Image
* ๐’ข๐‘’๐“ƒ๐‘’๐“‡๐’ถ๐“โ€™๐“ˆ ๐’ฏ๐‘’๐’ถ๐“‚ ๐“Ž๐’ถ ๐ฟ๐“Š๐‘”๐’ถ๐“๐‘œ ๐“Ž๐’ถ๐“€๐’พ๐“…๐’พ๐‘”๐’ถ ๐“€๐“Œ๐’ถ ๐“‚๐’ถ๐“‡๐’ถ ๐“Ž๐’ถ ๐“€๐“Œ๐’ถ๐“ƒ๐“๐’ถ ๐’ฎ๐‘’๐“‡๐‘’๐“ƒ๐‘”๐‘’๐“‰๐’พ. Na. Catherine Mbena, SERENGETI. Ujenzi wa mradi wa kimkakati wa uwanja wa gofu Hifadhi ya Taifa Serengeti โ€œSerengeti National Park Golf Courseโ€ uliobuniwa na Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania chini ya Mwenyekiti wake Jenerali (Mstaafu) George Waitara unaojengwa katika eneo la Fort Ikoma, nje kidogo ya Hifadhi ya Taifa Serengeti umefikia asilimia 42. Utekelezaji huo unajumuisha ujenzi wa โ€œTee and Greenโ€ kwa mashimo kumi na nane; mashimo tisa ya kwanza (front- nine/inbound holes),  mashimo tisa ya nyuma (back - nine/outbound holes), uchimbaji wa visima virefu viwili vyenye uwezo wa kutoa maji kiasi cha lita elfu kumi kwa saa kwa kila moja, uchimbaji na ujenzi wa mabwawa ya maji mawili yenye ujazo wa takribani lita millioni 22 kila moja, ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilomita 5.2 kuzunguka uwanja mzima, ujenzi wa โ€œpower houseโ€ na ufungaji wa...

KAMPENI YA TWENZETU KILELENI 2024 YAWAVUTA WAMAREKANI

Image
Na. Happiness Sam- Kilimanjaro  Wakati pazia la Twenzetu Kileleni msimu wa nne likiwa limefunguliwa rasmi leo Disemba 03, 2024 katika Lango la Lemosho lililopo wilayani Siha Mkoani Kilimanjaro, limevutia pia watalii kutoka Taifa la Marekani ambao wameungana na Watanzania wapatao 33 kwenda katika Kilele cha Mlima Kilimanjaro kuadhimisha miaka 63 ya uhuru wa Tanganyika ifikapo tarehe 09.12.2024. Akiwaaga wapandaji hao Mhe.Dkt Christopher David Timbuka Mkuu wa Wilaya ya Siha alisema, "Nimefarijika kuona idadi ya wapandaji imeongezeka kutoka watalii 11 waliopanda mwaka 2023 na kufikia wapandaji 33 mwaka huu 2024 ambapo idadi hii ni zaidi ya asilimia 100% huku zoezi hilo likiendelea kujizolea umaarufu na kuvuka mipaka ya Tanzania na kwenda mbali zaidi  kuvutia watalii kutoka Taifa la Marekani.โ€ Mhe. Dkt.Timbuka pia alitumia nafasi hiyo kumshukuru Mkurugenzi wa Kampuni ya African Scenic kwa kuipa hadhi njia ya Lemosho kuwa ni miongoni mwa njia inayotumika mwezi Disemba katika zoezi ...